Welcome.Karibu.Machiegni.

... happy you're here, finally. these random thoughts are random, the poetry is from pseudo -poets and any likeness to any human being, living or not so alive, is purely (well, mostly) coincidental. enjoy

11 June, 2010

KWAHERI-NI

Nazunguka hata napaa
Huku na kule nakaa
Nikiwaaga marafiki
Wajane waso manafiki
Warembo wa vitendo
Na mayatima wa kiakademia
Wao watakaosalia nanga ning'oapo

New York mjini hakunitoshi
Atlantic City mradi nielekee
Ila tu maCasino siingii
Itanikoma basi nauli
Kwani 'Ujaluoni' nako hakusalii kamwe
Washington DC kuingia
Kaka Barry kumgotea basi ni lazima

Kwaheri na makumbatio
Machozi na mate ya tamati
       yote siyapendi
Duniya tu ni barabara bali
Maisha hii kweli i safari

Mwendo wa kasi hapo awali
Sasa keshaingia tamati
Kujikokota tena siwezi
Ila bado fursa sipati

Na kusindikizwa kwa ajabu
Kweli raha ama huku tena hawanitaki
Mahenge tuandamane hadi Dubai
Daudi Nairobi ndiyo kikomo

Mtasemaje mlosema sitarudi?

No comments:

Post a Comment